Kutana na Shadrack ambaye alikuwa kijana mwenye ndoto kubwa za kimaisha. Alizaliwa na kukulia Moshi, mji wenye mandhari ya kuvutia chini ya mlima Kilimanjaro. Tangu akiwa mdogo, alitamani kuwa mfanyabiashara maarufu, mtu ambaye angeweza kujitegemea na kusaidia familia yake. Hata hivyo, safari yake ya kibiashara haikuwa rahisi.
Mara ya kwanza alipojaribu, Shadrack alifungua duka dogo la kuuza nguo za mitumba. Alijitahidi sana, akatafuta bidhaa bora na kuwekeza akiba yake yote. Lakini baada ya miezi michache, wateja wakaanza kupungua, na hatimaye duka likafungwa. Alijifariji akisema labda hakuchagua biashara sahihi.
Baada ya muda, alijaribu tena. Safari hii alianzisha mgahawa mdogo uliokuwa ukipika chakula cha kienyeji. Alikuwa na hamasa kubwa, akiamini watu wa Moshi na wageni wengi wangefurahia ladha ya chakula chake. Lakini mambo yalikwenda kinyume. Chakula kilikuwa kizuri, lakini kila mara alikumbwa na changamoto zisizoelezeka: vifaa kuharibika, wateja kupotea ghafla, na gharama kuongezeka bila sababu. Mgahawa nao ukafungwa..SOMA ZAIDI








No comments:
Post a Comment