MCHUNGAJI –MORAVIAN: WAZAZI TENGENI MUDA WA KUZUNGUMZA NA WATOTO WENU - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, November 30, 2025

MCHUNGAJI –MORAVIAN: WAZAZI TENGENI MUDA WA KUZUNGUMZA NA WATOTO WENU

Mchungaji Ester Mwasyoge Mwenyekiti wa Wilaya wa  Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kaskazini Dodoma (kushoto), akiwa pamoja na Mchungaji Ephraim Mbise wa kanisa hilo Usharika wa Nkuhungu wakati wa ibada ya sakramenti ya kipaimara na ubatizo iliyofanyika Novemba 30, 2025 jijini Dodoma.

Na Dotto Mwaibale, Dodoma

WAZAZI wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto ili kuzungumza nao masuala mbalimbali ya maisha yakiwemo maadili jambo litakalowasaidia katika maisha yao.

Ombi hilo limetolewa na Mchungaji Ester Mwasyoge Mwenyekiti wa Wilaya wa  Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kaskazini Dodoma wakati akihubiri katika ibada ya sakramenti ya kipaimara na ubatizo iliyofanyika Usharika wa Nkuhungu Novemba 30, 2025.a

“ Watoto wetu siku hizi wamekosa maadili kwa sababu wazazi wengi wanashindwa kutenga muda wa kuzungumza nao baba akitoka saa 11 aljfajiri akienda kwenye shughuli zake atarudi nyumbani saa nne usiku na kuwakuta wamelala na wakati mwingine inaweza kupita hata siku tatu hajaonana nao,” alisema Mwasyoge.

Alisema wazazi ndiyo wenye jukumu la kuwaelekeza watoto wao miongozo ya maisha yao na hasa kuzigatia maadili, heshima, unyenyekevu na masuala mengine yanayofanana na hayo yakiwemo  yanayohusu miili yao hasa kwa vijana walioingia kwenye umri wa kubalehe.

Akinukuu maneno ya Mungu kutoka Kitabu cha Kumbukumbu ya Torati 6:4-9 ambayo baadhi yake yanasema Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa nguvu zako zote.

“Na maneno haya ninayokuamuru leo yatakuwa katika moyo wako nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii na kuyanena uketipo katika nyumba yako na utembeapo njiani na ulalapo na uondokapo. Yafunge yawe dalili juu mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako, tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako na juu ya malango yako,” Mchungaji  Mwasyoge aliyanukuu maneno hayo kutoka katika biblia.

Alisema maneno hayo ni ya muhimu na yanaimarisha upendo baina ya watoto na wazazi na kuwa Mungu ni mmoja hakuna mwingine zaidi yake anayepaswa kuabudiwa.

Mchungaji Mwasyoge aliongeza kuwa wazazi wanatakiwa kuwafundisha watoto wao kuomba msamaha, kuhudhuria ibada za nyumbani na kanisani, kuwafundisha stadi za kazi ili waweze kujitegemea na kutokwepa majukumu yao.

Akisisitizia suala la maadili alisema watoto wengi hasa vijana wamekuwa hawajielewe na ndiyo maana baadhi yao wamekuwa na mihemuko na kufuata mikumbo na kujiingiza kwenye maandamano na hata wakiulizwa madai yao ni yepi hawayajui.

Mwasyoge aliwataka watoto hao kuwasikiliza wazazi na walezi wao na kuwatii na kueleza kuwa hivyo ndivyo Mungu anavyohitaji.

Katika hatua nyingine Mchungaji Mwasyoge aliwataka watoto wote ambao wapo darasa la sita kuanza kujiandikisha kwa ajili ya kuanza mtaala wa kipaimara badala ya kusubiri wakiwa darasa la saba kwani inakuwa vigumu kutokana na kukabiliwa na maandalizi ya mitihani.

Aidha, aliutaka uongozi wa kanisa hilo Usharika wa Nkuhungu kutengeneza mpango kazi utakao saidia kuepusha mgongano wa tarehe wa matukio makubwa yanayofanyika katika kanisa hilo ili kutoa fursa na makanisa mengine kushiriki kwenye matukio husika.

Mchungaji Ester Mwasyoge Mwenyekiti wa Wilaya wa  Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kaskazini Dodoma akihubiri katika ibada hiyo.
Mchungaji Ephraim Mbise wa kanisa hilo Usharika wa Nkuhungu Dodoma akisisitiza jambo katika ibada hiyo.
Watoto Benjamin Manase na Catherine Richard Skana wakiwa tayari kwenda kanisani kushiriki ibada hiyo.
Mtoto Benjamin Manase akiwa katika ubora wake kabla ya kupokea kipaimara
Mtoto Catherine Skana akiwa katika ubora wake kabla ya kupokea kipaimara.
Watoto wakiwa tayari kupokea kipaimara.
Watoto wakiwa katika ibada ya kupokea kipaimara.
Watoto wakiwa kwenye ibada hiyo. Kutoka kushoto ni Catherine Skana, Catherine Kefa, Florencea Mwasambili na Caroline Kefa.
Watoto hao wakionesha biblia baada ya kukabidhiwa.
Taswira ya ibada hiyo.
Waumini wakiwa kwenye ibada hiyo ya kipaimara.
Ubatizo kwa watoto ukifanyika.
Watoto waliobatizwa wakipata mbaraka.
Mtoto akikabidhiwa cheti chake baada ya kubatizwa.
Watoto wakiwa kwenye ibada hiyo. Kutoka kushoto ni Catherine Kefa, Catherine Skana na Jaqualine Nzowa.
Wana kwaya Kuu ya kanisa hilo Usharika wa Nkuhungu wakiwa kwenye ibada hiyo.
Watoto wa kipaimara wakiwa kwenye ibada hiyo.
Mtoto Benjamin Manase akipokea kipaimara.
Watoto wakiombewa wakati wa kupata kipaimara.
Mchungaji Ephraim Mbise akimpongeza mtoto Benjamin Manase kwa kupata kipaimara.
Watoto wakionesha furaha yao baada ya kupata kipaimara. Kutoka kushoto ni Catherine Kefa, Catherine Skana na Jaqualine Nzowa.
Mtoto Benjamin Manase akikabidhiwa cheti baada ya kupokea kipaimara.
Mtoto Stephano Nzowa akipongezwa na mdogo wake Moreen baada ya kupokea kipaimara.
Mtoto Catherine akikabidhiwa cheti baada ya kupokea kipaimara.
Watoto wakionesha vyeti vyao baada ya kupokea kipaimara.
Mtoto Catherine Kefa akivikwa shada na wazazi wake baada ya kupokea kipaimara.
Rose Michael (Maarufu Mama Elisafi) akimvika shada Mtoto Catherine Skana baada ya kupokea kipaimara.
Mtoto Denis Mwakilaba, akivikwa shada na mama zake wadogo baada ya kupokea kipaimara.
Mtoto Catherine Richard Skana, akiwa katika ubora wake baada ya kupokea kipaimara.
Christina Ndila akimpongeza mdogo wake Benjamin Manase baada ya kupokea kipaimara.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad