KIWANDA CHA KIBOKO PLASTICS LTD KIMBILIO LA WANANCHI NCHINI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, 4 January 2026

KIWANDA CHA KIBOKO PLASTICS LTD KIMBILIO LA WANANCHI NCHINI

Muonekano wa matanki yanayotengenezwa na Kiwanda cha Kiboko Plastics Ltd kilichopo Jijini Dar es Salaam

...................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam 

BIDHAA za Plastiki zinazotengenezwa na Kiwanda cha Kiboko Plastics Ltd Jijini Dar es Salaam zimekuwa kimbilio kubwa la wananchi kwa ajili ya kuzitumia kwenye shughuli za kilimo na ujenzi. 

Kiwanda hicho kimekuwa na mchango mkubwa kwa Taifa kutokana na kuzambaza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu kila kona ya nchi yetu. 

Baadhi wa wateja wanaonunua bidhaa kutoka katika kiwanda hicho wamesema wakekuwa wakizinunua kwa wingi  kutokana na ubora wake. 

“  Bidhaa za Kiboko Plastics ni nzuri na zina ubora wa hali ya juu matenki ninayoyatumia kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji nilinunua kwao hadi leo ninayatumia na sasa ni mwaka wa nne,” alisema Godlove Benard mkulima wa mbogamboga wilayani Handeni mkoani Tanga. 

Kwa upande wake Lusajo Hebron fundi bomba mkazi wa Mnada mpya jijini Dodoma anasema kutokana na ubora wa vifaa vinavyo tengenezwa na kiwanda hicho mahitaji ya baadhi ya vifaa na bomba za wateja wake kama PVC, HDPE Pipes, matenki ya maji, Poll Pipe na PPR Pipe amekuwa akinunua kupitia mawaka wao waliopo jijini humo.

Alitaja vifaa vingine ambavyo ananunua kuwa ni Flexbe pipe, Meelconecta, Ballgate na Nobel PN/ Elbaw Coupling.

Lusajo alisema tanki za kuhifadhia maji zinazotengenezwa na kampuni hiyo ni imara na salama kwa matumizi ya familia, hutunza maji kwa muda mrefu katika hali ya usafi na ubora wa hali ya juu na pia hayapasuki na jua, kuvuja, wala kupata kutu.

Kwa mujibu wa idara ya masoko ya kampuni hiyo inaeleza kuwa  ina Tank lita 3000 ambayo yanauzwa Sh. 400,000, tank lita 4000 ambalo zinauzwa Sh. 500,000,tank lita 6000 ambalo linauzwa Sh. 850,000, tank lita 8000 ambalo linauzwa Sh.1020,000 na tank lita 10000 ambali linauzwa Sh. 1,500,000.

Kwa mteja ambaye atanunua anaweza kupata punguzo la asilimia 40  pamoja na kusafirishiwa bure nchini kote na ukamilishwaji wa usafiri huo unakuwa ndani ya masaa 48.

Kwa maelezo zaidi ya kununua bidhaa hizo unaweza kuwasiliana nao kupitia ukurasa wao wa kibokoplastictz. simu namba  0712 773 336 au idara ya masoko sales@kibokoplastics.online na WhatsApp namba 0750866871.

Muonekano wa viungo vya mabomba vinavyotengenezwa na kiwanda hicho.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad