MBUNGE MGONTO AENDELEA KUCHANJA MBUGA ATOA VIFAA VYA MICHEZO SHULE ZA SEKONDARI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, January 27, 2026

MBUNGE MGONTO AENDELEA KUCHANJA MBUGA ATOA VIFAA VYA MICHEZO SHULE ZA SEKONDARI

Wanafunzi wakiwa kwenye maadhimisho ya miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Februari 5, 1977 yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yaliyofanyika Januari 26, 2026 wilayani Ikungi mkoani Singida.

......................

Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Jimbo la Ikungi Mashariki Mhe. Thomas Mgonto ameendelea kuchanja mbuga kwa kuwapelekea maendeleo wananchi wa jimbo hilo katika nyanja tofauti ambapo awamu hii ameigusa sekta ya elimu kwa kutoa vifaa vya michezo kwa  Shule za Sekondari ya Mungaa na Makiungu.

Hafla ya kukabidhi vifaa hivyo ni moja ya tukio katika  kuadhimisha miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Februari 5, 1977 yaliyofanyika wilayani Ikungi mkoani Singida Januari 26, 2026.

Maadhimisho hayo yalifanywa na Jumuiya ya Wazazi ya chama hicho Wilaya ya Ikungi chini ya Mwenyekiti wake Haji Kangaa ambaye alimwakilisha mbunge huyo aliyekuwa mgeni rasmi lakini hakuweza kushiriki kutokana na kuwa na majukumu mengine ya kikazi.

Mkangaa akizungumza katika maadhimisho hayo aliwahimiza wanafunzi wa shule hizo kusoma kwa bidii, kuwa na nidhamu ili waweze kutimiza ndoto za maisha yao pamoja na kuwa viongozi wa baadae.

Aidha, Kangaa aliwataka wazazi  na walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shuleni kwani ni haki yao ya msingi ya kupata elimu na hivyo kusiwepo na vikwazo vyovyote wakati wa kuwandikisha na hata kama hawatakuwa na sare za shule na mahitaji mengine wapokelewe.

Vifaa hivyo vya michezo vilikabidhiwa na Katibu wa mbunge huyo Hussein Mseule ni jezi na mipira.

Wajumbe wa Jumuiya hiyo walimshukuru na kumpongeza Mhe. Mgonto kwa jitihada zake anazozifanya za kuwatumikia.

Kwa upande wao wanafunzi wa shule hizo walimshukuru mbunge huyo kwa kuwapa vifaa hivyo ambavyo vitasaidia kuibua vipaji vya michezo.

Katika maadhimisho hayo zilifanyika shughuli zingine za kijamii ikiwemo kupanda miti ikiwa ni kumuunga mkono Rais wa Jamhuri yaa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye Januari 27, 2026 amesherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kupanda miche ya miti nyumbani kwake Kizimkazi Zanzibar. 

Viongozi wakiwaa mezaa kuu wakati wa maadhimisho hayo.
Mwenyekiti waa Jumuiya yaa Wazazi Wilayaa ya Ikungi, Haji Kangaa aakizungumza na wanafunzi

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM, Wilaya ya Ikungi, Haji Kangaa akiongoza shughuli ya kupanda miti.
Vifaa vya michezo vikikaabidhiwa.

 Vifaa vya michezo vikikaabidhiwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad