Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, Mhe. Daniel Sillo (wa pili kushoto), akipokea taarifa alipokuwa kwenye ziara ya kukagua ujenzi wa baadhi ya shule katika jimbo hilo.
.............................
Na Dotto Mwaibale
KIONGOZI bora ni yule anayefanya kazi kwa vitendo kwa ajili ya kuwatumikia wananchi na siyo kukaa ofisini na kuagiza wakuu wa idara au wasaidizi wake.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, Mhe. Daniel
Sillo hakika ni kiongozi wa vitendo zaidi mwenye kasi ya kuwatumikia wananchi.
Kutokana na kufanya kazi kwa
ratiba kasi ya utendaji wake inaongezeka kila siku ambapo jana Januari 3, 2026,
alifanya ziara ya kikazi katika Shule ya Sekondari ya Wavulana Manyara pamoja
na Shule ya Sekondari Kisangaji, kwa lengo la kukagua hatua iliyofikiwa katika
ukamilishaji wa mabweni ya wanafunzi wa kike na wa kiume katika shule hizo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Sillo
alikagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni yaliyogharimu jumla ya Sh. Milioni 260
shule ya sekondari Kisangaji, fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya
kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuishi wanafunzi.
Mhe. Sillo aliridhishwa na
matumizi ya fedha hizo pamoja na ubora wa kazi uliofanyika, akisisitiza umuhimu
wa kusimamia miradi ya maendeleo kwa uadilifu na thamani halisi ya fedha.
Aidha, alitembelea Shule ya
Sekondari ya Wavulana Manyara, mradi mkubwa wa elimu unaogharimu Sh. Bilioni
4.1.
Ameeleza kuwa kwa sasa
wanafunzi wa kidato cha tano tayari wanaendelea na masomo, huku wanafunzi wa
kidato cha kwanza wakitarajiwa kuanza masomo mwezi huu, hatua inayodhihirisha
dhamira ya Serikali ya kuimarisha elimu ya sekondari katika Mkoa wa Manyara.
Akizungumza na walimu na
viongozi wa elimu, Mhe. Sillo amewahimiza watendaji kuhakikisha wanakamilisha
miradi kwa wakati na kuitunza miundombinu iliyopo ili idumu kwa muda mrefu.
Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi
za Mbunge huyo kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jimbo la
Babati Vijijini, hususan ya sekta ya elimu.










No comments:
Post a Comment