Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kufungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi mkoani Singida Januari 15, 2026.
.....................
Na Mwandishi Wetu, Singida
WAFANYAKAZI wa Bodi ya
Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB)wamekutana mkoani Singida katika kikao cha
baraza la wafanyakazi kwa ajili ya kuweka mikakati ya pamoja namna ya kujadili
utendaji wa kazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB,
Godfred Mbanyi akizungumza na waandishi wa habari wakati akifungua kikao hicho
Januari 15, 2026 alisema watakuwepo kwa siku mbili mkoani Singida kwa ajili ya
kujadili mpango kazi wa kitaasisi pamoja na kufanya tathimini ya utendaji ya mwaka
uliopita na kuweka mkakati wa pamoja wamaboresho katika idara mbalimbali na
vitengo.
“Tunafanya kikao hiki ili
tuweze kuendana na sheria inayotuongoza kutekeleza majukumu yetu mbalimbali ya
Serikali,” alisema Mbanyi.
Mbanyi alisema baraza hilo
la wafanyakazi huwa linafanyika mara mbili na ni chombo cha kiuwakilishi na
kuwa katika kikao hicho kuna wakuu wa idara na vitengo vyote na kila kitengo
kimetoa mwakilishi mmoja mmoja wa kusikiliza na kuwasilisha mijadala ambayo
wataona inafaa kwa maboresho ya utendaji katika maeneo yao.
Alisema katika taasisi za
Serikali mabaraza hayo ya wafanyakazi yapo kwa mujibu wa sheria ya mahusiano
kazini na katika usimamizi wa ujumla wa kitaifa wapo chini ya ofisi ya waziri
mkuu.
“Katika kikao hiki
tutajadili utendaji wa nusu mwaka katika mwaka huu wa fedha wa 2025/ 2026
tuangalie tumefanya nini wakati tukijielekeza mwaka mpya wa fedha wa 2026/2027
na kuangalia maboresho zaidi na kuona tunaendaje,” alisema Mbanyi.
Alisema katika kikao hicho
pia watasikiliza maoni ya wafanyakazi ambao hawapo kwenye vikao vya maamuzi na
kuyapeleka kwenye vikao vya menejimenti kwa ajili ya kuyafanyia kazi.
Kwa upande wake mwakilishi wa vijana wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) katika bodi hiyo, Seif Musa alisema katika kikao hicho wanatarajia makubwa kwa yale watakayoyajadili na kuelekezwa na kufuata miongozo mbalimbali itakayopendekezwa.
Naye Nancy Mwamakimbula
Msimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala PSPTB amesema kupitia baraza hilo wanategemea
kupata maoni mengi ya wafanyakazi ya kuboresha utendaji wa kazi.
Alisema katika baraza hilo
pia watazungumzia masuala ya bajeti na maoteo ya bajeti ya mwaka ujao wa 2026/
2027 pamoja na utekelezaji wake.
“Kimsingi tunatarajia baraza
hili kuwa na manufaa sana kwetu hasa katika maboresho ya utendaji kazi na
kuboresha mambo yote ambayo watumishi wote watatamani yaboreshwe yanayohusu
taasisi na taaluma ya Ununuzi na Ugavi nchini.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Tawi La PSPTB-Dodoma. Shilla Mwandu akizungumza.

Afisa Rasilimali Watu na Utawala PSPTB, Nancy Mwamakimbula akizungumza
Kikao kikiendelea
















No comments:
Post a Comment