Naitwa Hamisi, mzaliwa wa mkoa wa Tabora lakini nilikuwa natafuta maisha jijini Dodoma kwa miaka mingi. Kazi yangu ilikuwa ni udereva wa bodaboda, kazi ambayo ilikuwa inanichosha mwili lakini mfukoni nabaki mkavu. Nilikuwa naamka saa kumi na moja alfajiri na kurudi saa tano usiku, lakini pesa niliyokuwa naingiza ilikuwa ni ya kula tu na kulipa kodi ya pikipiki ya bosi.
Maisha yalikuwa magumu kiasi kwamba mke wangu alishindwa kuvumilia na kuamua kunikimbia akidai mimi ni mwanaume “suruali” nisiye na mbele wala nyuma.
Hali hiyo ilinidhalilisha sana. Nilijihisi kama mwanaume aliyefeli kila idara. Kila nikijaribu kuweka akiba ili ninunue pikipiki yangu mwenyewe, dharura zilikuwa zinatokea na kuitafuna ile pesa yote. Nilianza kuhisi kuna mkosi umeniganda au labda nimerogwa na washindani wangu.

.jpg)






No comments:
Post a Comment