MIGODI MIKUBWA NCHINI IMETAKIWA KUWEZESHA WACHIMBAJI WADOGO - SINGIDANI BLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, 23 February 2026

MIGODI MIKUBWA NCHINI IMETAKIWA KUWEZESHA WACHIMBAJI WADOGO

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake mbele ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkoa wa Geita, Menejimenti ya Mgodi wa Geita na watendaji wa Ofisi yake katika ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML).


*************

Na Mwandishi Wetu

Wito umetolewa kwa makampuni makubwa ya uchimbaji madini nchini kuwekeza katikakuwawezesha wachimbaji wadogo katika nyanja mbalimbali ikiwemo teknolojia za kisasa na usimikaji wa mifumo ya usalama na afya mahali pa kazi ili kujenga uchumijumuishi unaotokana na sekta ya madini.

Wito huo umetolewa na serikali kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, alipofanya ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria yaUsalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi wa Dhahabuwa Geita (GGML).

Waziri Sangu ameipongeza menejimenti ya Mgodi huo kwa kuzalisha ajira nyingi kwaWatanzania ambapo GGML imeajiri jumla ya wafanyakazi 2,366 moja kwa moja na4,629 wameajiriwa kupitia wakandarasi mbalimbali wanatoa huduma katika Mgodi waGGML.

Sambamba na pongezi hizo, Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kazi ameutakaMgodi huo kuhakikisha kwamba shughuli zake zinakuwa na athari chanya katikauchumi wa jamii zinazowazunguka kwa kutoa fursa za kazi za muda mfupi ikiwemokuwezesha miradi mbalimbali ya kijamii.

Aidha, Waziri Sangu ameipongeza GGML kwa kuchagua suala la usalama na afya kwawafanyakazi kuwa tunu yao ya kwanza katika shughuli zao za uchimbaji na uchakatajiwa madini jambo ambalo limewafanya kujenga mifumo madhubuti ya kulinda afya nausalama wa wafanyakazi inayozingatia matumizi ya teknolojia za kisasa.

“Ninawapongeza kwa kuweka usalama na afya kama tunu yenu ya kwanza na hiiimejidhirisha katika wasilisho lenu mlilofanya hapa ambapo masuala ya usalama naafya yamechukua nafasi ya juu zaidi ya biashara mnayofanya,” ameeleza Waziri Sangu na kuongeza:

“Pongezi hizi inastahili pia Taasisi ya OSHA ambayo imekuwa ikiwaongoza katikakutekeleza hayo kupitia usimamizi mzuri wa Sheria Na.5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 na miongozo mbalimbali chini ya sheria hiyo ambayowamekuwa wakiitoa kupitia kaguzi zao za mara kwa mara.”

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita,Hashim Abdallah Komba, amesema OSHA ni miongoni mwa Taasisi zenye msaadamkubwa katika kuwezesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kufanyika kwa tija katikaMkoa wa Geita.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema ziara hiyo, inalenga kuona jinsi OSHA inavyoshirikiana na wadau wake kutekeleza Sheria yaUsalama na Afya mahali pa kazi ambayo dhima yake kuu ni kulinda nguvukazi ya Taifa dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi pamoja na kulinda uwekezaji kupitiakuzuia uharibifu wa mali.

Awali, menejimenti ya GGML iliwasilisha taarifa juu ya shughuli zao iliyoainisha jinsiafya na usalama wa wafanyakazi unavyozingatiwa katika shughuli husika. Miongonimwa masuala yaliyoelezwa katika taarifa hiyo ni pamoja na historia ya mgodi ambapoimeelezwa kuwa madini katika mgodi huo yaligunduliwa mnamo mwaka 1898 nauchimbaji rasmi kuanza mwaka 1999.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad