Nilianza kuamini kuwa mimi si wa kawaida.
Haikuwa kwa sababu nilikuwa na tabia mbaya au historia ya ajabu, bali kwa
sababu kila mwanaume niliyemruhusu aingie moyoni mwangu alikumbwa na msiba
mkubwa ndani ya mwaka mmoja.
Wengine walipoteza wazazi, wengine walipata
ajali mbaya, na mmoja alipoteza kazi na kuanguka kwenye msongo wa mawazo
uliomfanya anikimbie kabisa.
Mara ya kwanza nilidhani ni bahati mbaya tu. Tulikutana chuoni, tukapendana kwa dhati. Miezi nane baadaye baba yake alifariki ghafla. Alibadilika kabisa. Alianza kuniona kama mzigo wa ziada katika maisha yake yenye huzuni. Hatukudumu.








No comments:
Post a Comment