MKOA WA SINGIDA WAPOKEA TRILIONI 1.7 KWA AJILI YA MIPANGO YA MAENDELEO. - SINGIDANI BLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, 9 March 2026

MKOA WA SINGIDA WAPOKEA TRILIONI 1.7 KWA AJILI YA MIPANGO YA MAENDELEO.

Mkuu wa Mkoaa wa Singida, Halima Dendego akifungua Kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Singida kilichoketi Machi 8, 2026 mkoani humo.

.................................. 

Na Dotto Maibale, Singida


MKUU wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amesema  katika kipindi cha miaka minne iliyopita mkoa huo ulipokea Sh. 1.7 trilioni kwa ajili ya mipango ya maendeleo na usimamizi wa shughuli za Serikali.


Dendego aliyasema hayo wakati akifungua kikao cha kamati ya ushauri Mkoa wa Singida kilichoketi Machi 8, 2026 mkoani humo.


‘’ Katika kipindi cha miaka minne mkoa wetu umepokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo na usimamizi wa shughuli za Serikali tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkk. Samia Suruhu Hassan kwa kutupatia fedha hizo,’’ alisema Dendego.


Dendegu alisema Mkoa wa Sngida umeendelea kuwa na utulivu mkubwa kijamii na kisiasa na umeendelea kuwa salama na usalama mkubwa wa chakula kutokana na uzalishaji mkubwa unaofanywa na wananchi.


‘’ Na hata sasa Baraka za mvua  zimeendelea kuneemesha mazao yetu mashambani hivyo tunakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa Baraka hii kwani yapo maeneo hadi sasa mvua imekuwa kitendawili kikubwa,’’ alisema Dendego.


Alisema wote tumeshuhudia jinsi Serikali inavyoshirikiana na sekta binafsi, washirika wa maendeleo kwa kufanya vizuri sana kwenye mambo mengi yasiyotarajiwa kama vile kumpata Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigule Nchemba, Naibu Waziri-OR-Mipango na Uwekezaji Dkt. Pius Chaya na Balozi na Mshauri wa Rais –Diplomasia Mhe. Dkt. Lazaro Nyalandu.


Alitaja mambo mengine makubwa yasiyotarajiwa ni mkoa kumpata mwakilishi wa Bnge la Dunia Elibariki Kingu, mwakilishi wa Bunge la Afrika Mhe. Asha Feruzi na Maadhimisho ya Kitaifa ya Mei Mosi yaliyofana, kupokea Kombe la CECAFA kupitia timu yetu ya Singida Black Stars pamoja Mamlaka ya Mapato Tanzania '' TRA' kupata TUZO ya mkusanyaji bora wa mapato.


Aidha, Dendego alisema wastani wa pato la mkoa limeendelea kuongezeka japo si kwa kasi inayotakiwa na kwa sasa limefikia Sh. Trilioni 3.196 kutoka Sh.trilioni 2.700.


Alisema kwa wastani wa pato la mwananchi mmoja mmoja pia limeendelea kuongezeka kwa kufikia wastani wa Sh. 1,790,704 mwaka 2024/ 2025 kutoka Sh.1,588,605 mwaka 2020/ 2021 na kueleza kuwa pato hilo ni dogo  ukilinganisha na malengo ya Serikali kwenye Dira 2050.


Dendego aliongeza kuwa Mkoa wa Singida umeendelea kufanya vizuri kwenye ukusanyaji wa mapato kupitia TRA na Mapato ya ndani ya Halmashauri.

Katibu Tawala waa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Singida, Martha Mlata, akizungumza kwenye kikao hicho.
Wabunge wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Ikungi Magharibi, Elibariki Kingu, Mbunge wa Jimbo la Itigi, Yohana Msita na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Singida, Martha Gwau.
Viongozi wa dini wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kulia ni Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro na Chifu wa Mkoa huo,Mughenyi Senge Ndovu.
Mkuu waa Wilaya ya Manyoni Dkt. Vicent Mashinji aakichangia jambo kwenye kikao hicho.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa wa CCM Mkoa wa Singida, Diana Chilolo, akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Singida wakiwa kwenye kikao hicho.
Wenyeviti wa Halmashauri wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba  na Diwani wa Kata ya Kyengege Mhe.Innocent Msengi, Mwenyenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Tano Makambala.na Eliya Digha Mwenyekiti wa Wilaya ya Singida DC.
Taswira ya kikao hicho.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, Mohamed Juma Hamisi akiwa kwenye kikao hicho.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad