JUMUIYA YA WAZAZI CCM KIBONDO KUADHIMISHA WIKI YA WAZAZI 2026 KWA KUFANYA USAFI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, April 9, 2026

JUMUIYA YA WAZAZI CCM KIBONDO KUADHIMISHA WIKI YA WAZAZI 2026 KWA KUFANYA USAFI

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Kibondo, Evarist Mwonone.

..............................

 Na Dotto Mwaibale,

JUMUIYA ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma kesho kufanya maadhimisho ya wiki ya Wazazi 2026 kwa kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kufanya usafi.

Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 8, 2026 Katibu wa Jumuiya hiyo Wilaya ya Kibondo, Evarist Mwonone alisema maandalizi yote ya maadhimisho hayo yamekwisha kamilika.

“Maandalizi yote ya maadhimisho hayo yamekwisha kamilika pamoja na wageni waalikwa kuthibitisha kuhudhuria ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Hamisi Salum Tahiro,” alisema Mwonone.

Alisema maadhimisho hayo kiwilaya yatafanyika kesho Aprili 9, 2026 katika Kata ya Kizazi Tarafa ya Mabamba.

Katibu huyo wa jumuiya hiyo wilayaaani humo alisema maadhimisho hayo yatafanyika sambamba na shughuli za kijamii kama kufanya usafi maeneo ya Kituo cha Afya cha kata hiyo pamoja na kutoa misaada  kwa makundi mbalimbali ya watu wenye uhitaji wakiwemo wazee.

Alisema tukio hilo la utoaaji wa misaada hiyo litafanyika kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika katika kata hiyo ambapo alitumia nafasi hiyo kuwaalika wananchi wote kwenda kushiriki.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad