Pikipiki yangu ilikuwa zaidi ya chombo cha usafiri ilikuwa chanzo changu kikuu cha kipato. Nilikuwa naiitumia kila siku kufanya kazi na kujikimu. Siku moja niliiacha nje kwa muda mfupi tu, na niliporudi haikuwepo. Ilikuwa imeibwa.
Nilishtuka sana. Nilianza kuzunguka maeneo yote ya karibu, nikauliza watu, nikaripoti polisi, lakini hakuna aliyejua ilikoenda. Kila siku ilivyopita ndivyo matumaini yangu yalivyozidi kupungua. Nilianza kuhisi kama nimepoteza chanzo cha maisha yangu.








No comments:
Post a Comment