Maisha yangu yalikuwa yameanza kukaa vizuri. Biashara ilikuwa inaenda, pesa ilikuwa inaingia, na nilikuwa na mipango mingi ya maendeleo. Lakini ghafla mambo yalibadilika kwa kasi ambayo sikuitegemea. Mauzo yakaanza kushuka, wateja wakapotea, na hata miradi niliyokuwa nimepanga ilianza kufeli moja baada ya nyingine.
Nilijaribu kurekebisha hali kwa kuongeza juhudi, kubadilisha mikakati ya biashara, na hata kupunguza matumizi. Lakini kadri nilivyozidi kujitahidi, ndivyo mambo yalizidi kuwa mabaya. Ilifika hatua nikaanza kutumia akiba yangu hadi ikaisha kabisa. Nilihisi kama kila nilichogusa hakikuwa kinafanikiwa tena.








No comments:
Post a Comment