MKUU wa Mkoa
wa Singida, Halima Dendego amepongeza mapinduzi na mageuzi makubwa ya
kiutendaji yanayofanywa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), hususani mkoani
humo.
Mhe. Dendegu
ametoa pongezi hizo Aprili 30, 2026 wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vyombo
vya usafiri (Magari Manne) ya shirika hilo Mkoa wa Singida yaliyotolewa na
Serikali kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa kazi.
“Awali ya
yote nichukue nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali anayoingoza kwa jitihada kubwa anayoifanya
ya kuwajengea uwezo watumishi, kuwapeleka shule. kuongeza wafanyakazi wapya na
kuwaletea vitendea kazi, huu ni uwekezaji mkubwa unaofanywa ili muweze kufanya
kazi vizuri,” alisema Dendego.
Aidha,
alipongeza Tanesco Singida kwa kazi kubwa wanayoifanya chini ya Meneja wa
shirika hilo mkoani humo, Mhandisi Mwamvita Ally na timu yake na kueleza kuwa
tangia afike Singida hajawahi kuona changamoto kubwa ya umeme isipokuwa ile ya
kijumla.
Alisema
changamoto siku zote zipo, akitolea mfano mvua zinaponyesha nguzo zinaanguka na
nyingine nyingi lakini anafurahi anapoona zinapotokea wanapata taarifa na hatua
za kuzitatua zinapofanyika kwa wakati.
“Ikitokea
hitilafu tu mnatuambia na mnaifanyia kazi kwa wakati haya ni mapinduzi na
mageuzi makubwa ya kiutendaji ndani ya Tanesco chini ya Mkurugenzi Mtendaji Lazaro Twange,” alisema Dendego.
Aliongeza
kuwa hivi sasa umeme siyo anasa ni uchumi na ndiyo kila kitu hivyo
tunapotekeleza dira ya Taifa ya 20 / 50 malengo yetu yatafikiwa kwa nyinyi
kuhakikisha tunapata huduma ya umeme wa kutosha ambapo pia alihimiza magari
hayo yatunzwe.
Kwa upande
wake Meneja wa shirika hilo Mkoa wa Singida, Mhandisi Mwamvita Ally aliishukuru
Serikali chini ya Rais Samia kwa kuwapatia magari hayo ambapo aliahidi
kuyaatunza na kuhakikisha yatatumika kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.
Afisa
Usalama wa shirika hilo Mkoa wa Singida, Emilini Ndahani aliishukuru Serikali
kwa kuwapa magari hayo na kueleza kuwa watahakikisha yanatumika kwa kazi
iliyokusudiwa.
“Tunamshukuru
sana mkurugenzi wetu Lazaro Twange kwa jitihada alizofanya na kutupatia magari haya ambayo
yanakwenda kutoa huduma kwa wananchi na tutazingatia usalama wake pamoja na
watu kwa kuwaelekeza madereva matumizi bora ya magari hayo,” alisema Ndahani.
Naye
Mhandisi Boniface Shitindi wa shirika hilo Mkoa wa Singida alimshukuru Rais
Samia kwa kuwashika mkono na kuweza kutoa magari hayo ambayo yanakwenda kuwapa
tija ya kikazi.
“ Jambo ili
kwetu ni chachu ya kuongeza uchumi wa Taifa letu kama kauli mbiu yetu inavyo
sema “Tunayaangaza Maisha” ndivyo tunavyoendelea kuyaangaza kupitia magari hayo
tuliyopatiwa na Serikali.
Vyombo vya
usafiri vilivyo kabidhiwa ni Land Cruiser mbili mpya na mashine mbili za kuinua
vitu vizito zikiwemo nguzo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, akizungumza kwenye hafla hiyo.
Meneja wa shirika hilo Mkoa wa Singida, Mhandisi Mwamvita Ally akizungumza.
Afisa Usalama wa shirika hilo Mkoa wa Singida, Emilini Ndahani, akizungumza.
Mhandisi Boniface Shitindi wa shirika hilo Mkoa wa Singida, akizungumza.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego (katikati), akiwa na viongozi wa shirika hilo wakati wa hafla hiyo.
Vyombo vya usafiri vilivyokabidhiwa.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990.









No comments:
Post a Comment