𝐓𝐔𝐌𝐄 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐈𝐏𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐊𝐔𝐉𝐄𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐈𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐈𝐌𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐀 𝐓𝐀𝐓𝐇𝐌𝐈𝐍𝐈 𝐔𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐈𝐑𝐀 𝟐𝟎𝟓𝟎 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, May 5, 2026

𝐓𝐔𝐌𝐄 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐈𝐏𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐊𝐔𝐉𝐄𝐍𝐆𝐀 𝐌𝐈𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐈𝐌𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀𝐉𝐈 𝐍𝐀 𝐓𝐀𝐓𝐇𝐌𝐈𝐍𝐈 𝐔𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐈𝐑𝐀 𝟐𝟎𝟓𝟎

Na Mwandishi Wetu, Kibaha-Pwani.

Imeelezwa kuwa Tume ya Taifa ya Mipango imekamilisha nyenzo zote za utekelezaji wa Dira 2050 ambazo ni Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051 (LTPP 2050), Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2026/27 – 2030/31 (FYDP IV) na Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2026/2027 kuelekea Julai 1, 2026 ambapo utekelezaji wa Dira hiyo utaanza rasmi.

Hayo yameelezwa leo Mei 4, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango Dkt. Tausi Kida alipofungua mafunzo kwa Wakurugenzi wa Sera na Mipango, Wakurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini, na Wakuu wa Idara na Vitengo vya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali yanayofanyika katika Chuo cha Uongozi Mwalimu Julius Nyerere, Kibaha - Pwani.

Dkt. Kida amewaambia washiriki wa mafunzo hayo kuwa, baada ya kukamilisha Dira 2050 na nyenzo zake, mafunzo hayo ni utekelezaji wa mkakati mahususi wa Serikali wa kujipanga kufanya utekelezaji wa Dira hiyo kwa kuhakikisha kunakuwepo na uelewa wa pamoja na utekelezaji unaolingana katika ngazi zote za Wizara, Taasisi za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuhakikisha mipango ya Kitaifa inatekelezwa kwa tija.

“ Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Mipango inakamilisha Miongozo ya Upangaji (NPGs), Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Programu na mirado ya Maendeleo (NF-MEDeP) na Mfumo wa Kidigitali uitwao E-Delivery. Mfumo huu na miongozo hiyo italetwa kwenu na mafunzo stahiki yanaandaliwa kwa ajili yenu” Amesisitiza Dkt. Kida.

Aidha, Dkt. Kida amesema kupitia mafunzo hayo, washiriki watapata fursa ya kujifunza kwa vitendo (i.e. case studies), kubadilishana uzoefu, na kujenga uwezo katika hatua zote za mzunguko wa miradi ya maendeleo kuanzia uibuaji, upangaji, uchambuzi, uidhinishaji hadi utekelezaji na ufuatiliaji.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad