Kwa miaka mingi nilikuwa naishi na maumivu ambayo si rahisi kuelezea. Kila nilipoona watu wakisherehekea ujauzito au watoto wao, nilijikuta nikitabasamu kwa nje lakini moyoni nikiumia sana. Ndoto yangu kubwa ilikuwa kuwa mama, lakini kadri miaka ilivyopita, matumaini yangu yalizidi kufifia.
Nilijaribu kila nilichoweza. Nilitembea hospitali tofauti, nikafanya vipimo vingi, na kufuata matibabu niliyoelekezwa. Kila nilipoambiwa “endelea kuwa na matumaini,” nilijikaza. Lakini kila mwezi ulipopita bila mabadiliko, machozi yangu yaliongezeka.









No comments:
Post a Comment