RC SINGIDA AWAPONGEZA WAFANYAKAZI MEI MOSI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, May 2, 2026

RC SINGIDA AWAPONGEZA WAFANYAKAZI MEI MOSI

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, akiwahutubia wafanyakazi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kimkoa Uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida.

............................

MKUU wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, amewapongeza Wafanyakazi wa mkoa huo kwa mchango wao mkubwa wa maendeleo.

Mhe. Dendego ambaye alikuwa mgeni rasmi alitoa pongezi hizo wakati akiwahutubia wafanyakazi hao kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kimkoa Uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida.

“ Nitumie maadhimisho haya kuwa pongezeni kwa mchango wenu mkubwa wa kuuletea maendeleo mkoa wetu na hayo ndiyo matokeo ya ushirikiano wa pamoja mlionao,” alisema Dendego. 

 Mhe. Dendego aliongeza kuwa dhamira ya Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuboresha mazingira ya kazi na mafanikio ya maendeleo yanategemea ustawi wa wafanyakazi.

Akizungumzia changamoto zilizowasilishwa kupitia risala ya wafanyakazi hao aliahidi kuzifanyia kazi  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Mkoa wa Singida, Agness John alimpongeza Rais Samia kwa kutekeleza ahadi aliyoitoa Julai 2025 ya kuongeza mshahara kwa wafanyakazi wote nchi nzima ikiwa ni pamoja na kuwapa kicheko kwa kuwaboreshea miundombini ya kufanyia kazi.

“Miundombinu mizuri ya kufanyia kazi imekuwa ikiwarahisishia wafanyakazi kufanya kazi kwa furaha ndiyo maana nimesema amekuwa akiwapa kicheko kwenye maslahi, mazingira ya kufanyia kazi na maeneo mengine,” alisema John. 

Naye Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Singida, Deogratius Lugambwa alisema kuwa shirikisho hilo litaendelea kutoa ushirikiano wote unaostahili kupitia vyama shiriki mkoani humo.

“Dhamira ya shirikisho letu ni kuhakikisha tunakuwa kiunganishi imara kati ya mwajiri na mfanyakazi kwa ajili ya tija ya taifa na mkoa wetu wa Singida,” alisema Rugambwa.

Alisema shirikisho hilo linaendelea kutoa elimu ya kutosha kuhusu haki wajibu wa mfanyakazi ili kila mmoja atomize majukumu yake kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma kwa wale walioajiriwa katika utumishi.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Mkoa wa Singida, Agness John, akizungumza.

Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Singida, Deogratius Lugambwa, akizungumza.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye maadhimisho hayo.

Maonyesho ya kazi mbaalimbali yakipita mbele ya jukwaa kuu.

Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzaania (TANESCO), Mkoa wa Singida wakipita mbele ya jukwaa kuu.
Maandamano yakipita jukwaa kuu.

Maandamano yakiendelea kupita mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Hlima Dendego.

Maandamano yakiendelea

Taswira ya maadhimisho hayo
Wimbo wa mshikamaano ukiimbwa.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad