............................
MKUU wa Mkoa
wa Singida, Halima Dendego, amewapongeza Wafanyakazi wa mkoa huo kwa mchango
wao mkubwa wa maendeleo.
Mhe. Dendego
ambaye alikuwa mgeni rasmi alitoa pongezi hizo wakati akiwahutubia wafanyakazi
hao kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani (Mei Mosi)
yaliyofanyika kimkoa Uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida.
“ Nitumie maadhimisho haya kuwa pongezeni kwa mchango wenu mkubwa wa kuuletea maendeleo mkoa wetu na hayo ndiyo matokeo ya ushirikiano wa pamoja mlionao,” alisema Dendego.
Mhe. Dendego aliongeza kuwa dhamira ya
Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuboresha
mazingira ya kazi na mafanikio ya maendeleo yanategemea ustawi wa wafanyakazi.
Akizungumzia
changamoto zilizowasilishwa kupitia risala ya wafanyakazi hao aliahidi
kuzifanyia kazi kwa kushirikiana na
wadau mbalimbali.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Mkoa wa Singida, Agness John alimpongeza Rais Samia
kwa kutekeleza ahadi aliyoitoa Julai 2025 ya kuongeza mshahara kwa wafanyakazi
wote nchi nzima ikiwa ni pamoja na kuwapa kicheko kwa kuwaboreshea miundombini
ya kufanyia kazi.
“Miundombinu mizuri ya kufanyia kazi imekuwa ikiwarahisishia wafanyakazi kufanya kazi kwa furaha ndiyo maana nimesema amekuwa akiwapa kicheko kwenye maslahi, mazingira ya kufanyia kazi na maeneo mengine,” alisema John.
Naye Mratibu
wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Singida,
Deogratius Lugambwa alisema kuwa shirikisho hilo litaendelea kutoa ushirikiano
wote unaostahili kupitia vyama shiriki mkoani humo.
“Dhamira ya shirikisho letu ni kuhakikisha tunakuwa kiunganishi imara kati ya mwajiri na mfanyakazi kwa ajili ya tija ya taifa na mkoa wetu wa Singida,” alisema Rugambwa.
Alisema shirikisho hilo linaendelea kutoa elimu ya kutosha kuhusu haki wajibu wa mfanyakazi ili kila mmoja atomize majukumu yake kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma kwa wale walioajiriwa katika utumishi.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Mkoa wa Singida, Agness John, akizungumza.Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Mkoa wa Singida, Deogratius Lugambwa, akizungumza.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
Maonyesho ya kazi mbaalimbali yakipita mbele ya jukwaa kuu.
Maandamano yakiendelea kupita mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Hlima Dendego.
Maandamano yakiendeleaTaswira ya maadhimisho hayo
Wimbo wa mshikamaano ukiimbwa.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.



















No comments:
Post a Comment