TAASISI ya Asia Halamga Foundation chini ya Mhe
Asia Halamga Mbunge wa vijana Taifa leo
tar 21.12.2023 imekabidhi majiko ya gesi 50
kwa lengo kusaiidia waathirika wa maporomoko ya tope Wilaya ya Hanang,
Mbunge huyo ambaye, hivi karibuni alikabidhi mahindi gunia 10 kwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang' Janeth Mayanja ameendelea kutoa mkono wa pole pole kwa Wana Hanang kwa vitendo na kuahidi kuendelea na zoezi hilo hadi ndugu, jamaa, na marafiki walioathirika kurejea kwenye hali zao za kawaida na kushiriki shughuli za maendeleo kama ilivyokuwa awali.
Akipokea maada huo Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Athuman Likeyekeye alisema wanamatumaini makubwa na mbunge huyo ambaye ameonesha kwa vitendo na kutekeleza kwa nafasi yake kwa kuwakimbilia wananchi waliopatwa na athari za maporomoko ya tope wilayani Hanang'.
"Kitendo alichofanya Mbunge huyu ni cha kibinadamu na uzalendo mkubwa kwani ameunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha waathirika wa tukio hili wanapata mahitaji ya kibinadamu na ni ibada kubwa amefanya," alisema Likeyekeye.








No comments:
Post a Comment