Mbunge wa Iramba Mashariki, Mhe.Francis Isack Mtinga, akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Mbuyuni wakati alipokuwa kwenye hafla ya kukabidhi radio kwa wanawake Wachuja Nafaka katika tukio lililofanyika jana, Iguguno wilayani Mkamalama mkoani Singida.
Na Dotto Mwaibale, Singida
MBUNGE wa
Jimbo la Iramba Mashariki, Mhe.Francis Isack Mtinga ametimiza ahadi yake kwa
kutoa radio kwa Wajasiriamali Wanawake wanaojishughulisha na uuzaji wa pombe za
asili (WACHUJA NAFAKA) inayotengenezwa
kwa kutumia nafaka wa Kitongoni cha Mbuyuni Kata ya Iguguno wilayani Mkalama
mkoani Singida.
Akizungumza jana wakati akikabidhi radio hiyo
Mtinga alisema wanawake hao walikuwa na changamoto ya kukodi radio kila siku
walipokuwa wanafanya biashara yao ya kuuza pombe hiyo ya asili kwa ajili ya
kuwaburudisha wateja wao na kusababisha kupata kipato kidogo.
Alisema wanawake hao walimuomba awasaidie kununua
radio hiyo ili waondokane na changamoto ya kukodi radio kila wakati wanapokuwa
kwenye biashara yao.
"Leo siku ya Boxing Day nimeona nifike kwa
ajili ya kutekeleza ahadi yangu ya kuwapa radio itakayowasaidia kuwaburudisha
wateja wenu hivyo kuongeza kipato chenu kwa kuzingatia kuwa ninyi ni jeshi
kubwa na mnategemewa na watu wengi,” alisema Mtinga.
Baadhi ya wachuja nafaka hao walimshukuru mbunge
huyo kwa kutekeleza ahadi yake hiyo na kumuelezea kuwa ni mbunge anayejali
wananchi wake wote kwa ujumla.
“Mbunge wetu Mtinga ni mtu wa vitendo zaidi na kama mnavyoona katuleetea radio ambayo itakuwa ikitupa burudani wakati tunapata kinywaji chetu cha asili pamoja na kutuhabarisha mambo mbalimbali ya maendeleo,” alisema mmoja wa wanawake hao wachuja nafaka.










No comments:
Post a Comment