.........................................
Na Mashaka Kibaya, Tanga.
KOROGWE Mji, Handeni, Pangani na Muheza ni maeneo
ambayo Wananchi wake watanufaika na Mradi mkubwa wa Maji unaofahamika kama
Mradi wa Miji 28.
Mradi wa Maji wa Maji wa Miji 28 unaotarajiwa
kuyekelezwa hapa nchini Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia
Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi ili kuwaondoshea kero kwa Wananchi wake.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
ilipata mkopo nafuu kutoka Serikali ya India Kiasi cha Dola 500 Milioni
zimetolewa kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Maji wa Miji 28 nchini.
Aidha Mamlaka ya Maji Safi Handeni Trunk Main
(HTM) ni sehemu ya utekelezaji Mradi wa Miji 28 ambapo watatekeleza mradi
utakaohudumia Miji mine ya Handeni,
Korogwe, Muheza na ule wa Pangani.
Yohana Stephen Mgaza ni Mhandisi na Mkurugenzi
Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira, Handeni Trunk Main
(HTM) Wilayani Handeni.
Katika mazungumzo yake na Mwandishi wa Makala haya,
Mhandisi Mgaza alisema kwamba, kwa upande wa Korogwe, Handeni, Pangani na
Muheza Mradi utagharimu dola 81 Milioni ambazo ni zaidi ya Shilingi 200
Billioni hadi mradi kukamilika.
"Ni mradi mkubwa ambao tunategemea
kuusimamia kwa makini ,ni fedha nyingi sana ya Serikali itatumika"alisema
Mgaza huku akibainisha kuwa mradi huo utakuwa na chanzo kimoja ambacho ni Mto
Pangani.
Kutoka Mto Pangani Maji yatachukuliwa kwenye eneo
la Kijiii cha Mswaha Darajani, yatasafirishwa mpaka Kijiji cha Tabora
kutakakojengwa mtambo wa kisasa kuchuja Maji.
Baada ya hapo ndipo Maji yatatawanywa kwenda
maeneo mbalimbali katika Miji ya Handeni, Korogwe, Pangani na Muheza
kutakakojengwa matenki makubwa kwa ajili ya kuhifadhia Maji hayo.
Katika Mji wa Handeni tenki lenye ujazo wa lita
Milioni mbili litajengwa, Muheza tenki la lita milioni mbili, Pangani
kutajengwa matenki ya ujazo lita 500,000 Kijiji cha Boza,lita 300,000 Kijiji
cha Madanga na tenki jingine la lita laki mbili kujengwa kwenye Kijiji cha
Ubangaa.
Mradi wote huo urefu wake ni Kilomita 189 kutoka
kwenye Chanzo mpaka kufikia maeneo ya matenki ambayo yanakwenda kuwahudukia
Wananchi.
Mkurugenzi Mtendaji huyo wa HTM (Mgaza) alisema
kwamba, kwa kuanzia yatajengwa mabomba ya kusambaza maji kwenye urefu wa
Kilomita 100 maeneo yote ya Miji na baadaye kazi ya uaambazaji maji kwa
Wananchi itaendelea.
M/s JWIL Infra Construction Limited ndiye
Mkandarasi anayetekeleza Mradi huo akisimamiwa na Mtaalam Mshauri Kampuni ya
Wapcos zote za kutoka nchini India.
HTM inabakia kuwa Wataalam wa Wizara ya Maji
wakiwa Wasimamizi kuhakikisha mradi unajengwa kwa viwango ambavyo umefanyiwa
Usanifu kazi ambayo Mhandisi Yohana Mgaza ameahidi kuitekeleza.
Mradi huo unatarajiwa kuhudumia zaidi ya Watu
600,000 kwenye Miji hiyo ya Pangani, Korogwe, Muheza na Handeni huku Wananchi
watakaokuwa Vijiji vilivyo umbali wa Kilomita 12 kutoka bomba kuu popote
litakapokuwa linapita wakitarajiwa kunufaika.
Tayari mkabdarasi yuko eneo la Mradi anaelezwa
kuendelea na kazi akilaza mabomba kwenye maeneo mbalimbali ambapo kuna kipande
cha kutoka tenki la Korogwe kielekea Tabora kwenye Chujio alikoanza kulaza
bomba.
Pia mkandarasi ameanza kulaza bomba kutoka Kijiji
cha Komsala kuelekea Kijiji cha Mandela na kutoka Mandela kuelekea kwenye
Kijiji cha Masatu.
Vilevile mabomba mengine yamelazwa kwenye Kijiji
cha Tabora kuelekea Mji wa Korogwe huku ujenzinwa matenki ukiwa umeanza na
yaliyopo hatua ya kukwaga zege ni lile la Kijiji cha Madanga na Boza wilayani
Pangani.
Kwingine kazi ya kusafisha maeneo inaendelea ili
ujenzi kuanza rasmi huku ujenzi ukitarajiwa kuanza tenki la Vibaoni Handeni na
kusafisha eneo la kujenga Chujio Tabora.
Usafishaji unaendelea eneo la kujenga Chanzo
Mswaha ambapo kazi inaendelea vizuri ambapo Mhandisi Yohana Mgaza anaishukuru
Serikali ya awamu ya Sita kufikia malengo ya kupata fedha za kutekeleza mradi
utakaonufaisha Wananchi walio wengi.
Pongezi nyingine zinakwenda kwa Waziri wa Maji
Jumaa Aweso kwa juhudi zake za kuhakikisha mradi unafanyika ambapo Wataalam wa
HTM wameahidi kutokuwa kikwazo na mradi utajengwa kwa viwango stahiki.
"Sisi kama Wataalam wa HTM tukiwakilisha
Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo, tutahakikisha mradi unajengwa kwenye viwango
stahiki na kukamilika kama ulivyopangwa"alisema Mhandisi huyo wa HTM.
Mgaza hakusita kuzungumzia suala la
usiirikishwaji Wananchi kwenye Mradi akisema,kabla utekelezaji kuanza
walishirikiana na Viongozi wa vijiji, kata tarafa Chama na Serikali kupita
maeneo yatakayoguswa na mradi.
Uhakiki wa Wananchi wenye maeneo yenye mazao
umefanyika ili kufidiwa na kusikokuwa na mazao wameombwa ili kuweza kufanikisha
kufika kulikokusudiwa.
Mradi huo ulioanza Aprili 2023 unatarajiwa
kukamilika ifikapo Disemba 2024 ingwa awali ilikuwa iwe Disemba 2025 ambapo
unafanyika kwa njia ya Usanifu na ujenzi.
Hayo yamejiri baada ya kuonekana umuhimu na
mahitaji makubwa kwenye maeneo ya wananchi ambapo HTH iliketi na wataalam
washauri na wakandarasi kupitia mpango kazi wa utekelezaji na hivyo kujiwekea
malengo.
Mradi huo wa Miji 28 kwa Wilaya za Handeni,
Pangani, Korogwe na Muheza unaonekana kuwa fursa ya kujikwamua kiuchumi kwa
wananchi kwenye maeneo kazi zitakakofanyika.
Kipaumbele kutatolewa jwa wenyeji kushiriki shughuli za mradi ambapo vijana wamehamasishwa kujitokeza huku Mhandisi Yohana Mgaza akisema akina Mama pia wanaweza kujitokeza kwa biashara ya chakula.








No comments:
Post a Comment