SHEIKH SINGIDA ANUSURU MSIKITI WA BAKWATA KUPORWA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, 31 December 2023

SHEIKH SINGIDA ANUSURU MSIKITI WA BAKWATA KUPORWA

Sheikh Mkoa wa Singida, Issa Nasoro, akizungumza Disemba, 29, 2023 na Waislam wa  Msikiti wa Ijumaa wa Tarafa na Kata ya Mtinko unaosimamiwa na Baraza Kuu la Waislam  Tanzania (BAKWATA) kufuatia taasisi moja ya kiisilam kudaiwa kufanya mchakato wa kusajili umiliki wa msikiti huo ikitaka kuuchukua wakati ni mali ya Bakwata. 

(PICHA ZOTE NA SOLOMON PHILEMON)

.......................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

SHEIKH Mkoa wa Singida, Issa Nasoro amenusuru kuporwa kwa Msikiti wa Ijumaa wa Tarafa na Kata ya Mtinko unaosimamiwa na Baraza Kuu la Waislam  Tanzania (BAKWATA) kufuatia taasisi moja ya kiisilam kudaiwa kufanya mchakato wa kusajili umiliki wa msikiti huo ambao ni mali ya Bakwata.

Akizungumza na waandishi wa habari pamoja na waumini wa dini ya kiislam Disemba 29, 2023 kwenye msikiti huo, Sheikh Nasoro ambaye alikuwa ameongozana na Mwanasheria Mkuu wa Bakwata Taifa, Hassan Fatihu alisema kuna watu wamejitokeza kutengeneza taasisi ndani ya taasisi.

“Tumekuja hapa baada ya kuwepo kadhia kutokana na watu kujitokeza kwa ajili ya kupata usajili kupitia jengo la msikiti huu tunao ujenga ambao ni mali ya Bakwata na jiwe lake la msingi liliwekwa na Hayati Mufti Sheikh Mkuu, Hemed Bin Juma Bin Hemed Oktoba 28, 1990,’’ alisema Sheikh Nasoro.

Sheikh Nasoro alisema watu hao waliwarubuni viongozi wa msikiti huo ambao walikuwa hawajui chochote na  mara moja walianza mchakato wa kusajili msikiti huo kupitia taasisi yao huku wakijua ni mali ya Bakwata.

Alisema baada ya kubaini jambo hilo waliwasiliana na mamlaka mbalimbali na kufanikiwa kuzuia mchakato huo baada ya viongozi wa msikiti huo kubaini kuwa walikuwa wamerubuniwa na watu hao.

Mwanasheria wa Bakwata, Hassan Fatihu alisema msiki huo uliojengwa tangu mwaka 1945 ni mali ya Bakwata na si vinginevyo ambapo aliwataka viongozi wa dini hiyo kujenga tabia ya kuuliza jambo wasilolijua ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima kama huo ambao umemsikitisha.

Muumini wa Msikiti huo, Juma Mene alisema watu hao sio mara yao ya kwanza kuanzisha mgogoro huo kwani miaka ya nyuma walifungua kesi iliyodumu zaidi ya miaka 20 ambayo iliipa ushindi Bakwata na anashangaa kuona siku za hivi karibuni ukiibuka tena.

Mmoja wa Wajukuu wa waasisi wa msikiti huo alisema katika Tarafa hiyo hakuna muumini yeyote wa dini ya kiisilam asiyejua kama msikiti huo ni mali ya Bakwata hivyo hata kubali kuona kundi fulani likitaka kuuchua labda wawaue kabla kufanya hivyo.

Mwanasheria wa Bakwata, Hassan Fatihu, akizungumza kwenye tukio hilo.
Katibu wa Baraza la Masheikh Mkoa wa SingidaSaid Ally Mang'ola, akichangia jambo kwenye tukio hilo lililofanyika katika Msikiti wa Kata ya Mtinko.
Kikao hicho kikiendelea.
Muonekano wa jengo la Msikiti huo mali ya Bakwata ambalo linagombaniwa na taasisi hiyo.

ANGALIA VIDEO CHINI

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad