WANACHAMA 442 ILULU SACCO's MKOA WA LINDI WAKOPESHWA MILION 726.5 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, 27 December 2023

WANACHAMA 442 ILULU SACCO's MKOA WA LINDI WAKOPESHWA MILION 726.5

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga akizungumza na Wanachama wa Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Ilulu SACCO'S wakati akifungua mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika mkoani humo.

..................................... 

Na Said Hauni, Lindi.

 

CHAMA cha Ushirika cha Akiba na Mikopo cha Ilulu  SACCO'S Manispaa ya Lindi,kimekopesha kwa wanachama 442 kati ya 672 mikopo yenye thamani ya Sh,726,500,000 ikiwemo ya kilimo kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Mwenyekiti wa Chama hicho Yusufu  Nadeng'u ameeleza hayo alipokuwa anawasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi hicho katika mkutano mkuu wa 17 uliofanyika mjini Lindi.

Akiwasilisha taarifa yake hiyo, Nadeng'u amesema mikopo hiyo imehusisha shughuli za kilimo,vyombo vya usafiri,vikundi na vikundi vya wajasiliamali imetolewa Disemba 17/2022 hadi Disemba 16 mwaka huu.

Alisema mikopo iliyotolewa wapo wafanyabiashara wa kati na wadogo,wanachama wanaojihusha na kilimo,wajasilimali na waendesha pikipiki na kufanya jumla ni Sh,726,500,000.

Mwenyekiti huyo amewaeleza wajumbe wa mkutano huo Sh,94,500,000/= zimetolewa kwa waendesha pikipiki,sh,35,400,000, kilimo Sh,12,600,000 vikundi vya wajasiriamali na Sh,15,250,000 zilizobaki zimeenda kwa wafanyabiashara wadogo na wakati.

Alisema kati ya mikopo uliokopeshwa jumla ya sh,614,200,157/_zimeanza kurejeshwa na kufanya kiasi kilichobaki mikononi mws waliokopeshwa ni sh,107,112,842.

Nadeng'u alisema licha ya mafanikio hayo,bado  chama kina madeni sugu yenye thamani ya sh,20,885,222/_kati ya hizo baadhi ya wanachama wameweza kurejesha kwenye chama Sh 8,120,120/_na kufanya kiasi kilichosalia ni  sh,22,765,102.

"Pamoja na changamoto zilizopo baadhi ya wanachama wetu kutorejesha kwa wakati mikopo wanayochukuwa chama kimeendelea kupata faida, "alisema Nadeng'u.

Alisema katika kipindi hicho chama kimeweza kuongeza idadi ya wanachama kutoka 621 hadi 672 sanjari na kupata cheti na tuzo bora Mkoa wa Lindi mwaka 2023.

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga akizungumza na wanachama hao wa Ilulu SACCO'S amewataka waendelee kuwa wamoja kwa kuwapa ushirikiano mzuri kwa maendeleo ya chama chao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad