·Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Kisare Makori, akiongoza hafla ya uzinduzi wa matumizi ya nishati safi na salama inayotokana na makaa ya mawe iliyoandaliwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.
.........................
Na Mwandidhi Wetu, Mbinga
MKUU wa Wilaya ya Mbinga Kisare Makori amezindua matumizi ya nishati safi na salama InaYotokana na makaa ya mawe kwa ajili ya matumizi katika shule za msingi na sekondari za Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.
Hafla hiyo ya uzinduzi iliyoandaliwa na Halmashauri
ya Wilaya ya Mbinga imefanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana
Mbinga iliyoko Kata ya Kingonsera.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
Serikali, v kisiasa akiwemo Katibu wa CCM Wilaya ndugu Madodi, viongozi wa dini
akiwemo Askofu wa Jimbo Kuu la Mbinga,
John Ndimbo na Sheikh wa wilaya,, sekta binfsi na makampuni yanayochimba makaa
ya mawe.
Awali akitoa taarifa ya mkakati wa halmashauri
katika utekelezaji wa maelekezo ya serikali kuhusu matumizi ya nishati safi
kwenye maeneo yanayotoa huduma ya chakula kwa zaidi ya watu 100, Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Joseph Kasusura ameeleza kuwa
lengo la halmashauri ni kuhakikisha kuwa shule zote za msingi na sekondari katika
Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga zinatumia nishati mbadala iliyo safi na salama.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya
Mbinga Kisare Makori alisema "Suala la matumizi ya nishati safi ni jukumu
la kila mmoja katika ngazi za familia, taasisi na hata katika vikundi
mbalimbali"
Makori alisema changamoto za matumizi ya nishati chafu
na isiyo salama imekuwa ikionekana wazi katika nyanja mbalimbali za kijamii,
kiuchumi, kiafya na kimazingira ikiwemo ongezeko la ukataji miti ovyo.
Alisema vitendo hivyo vinachangia katika
mabadiliko ya tabia nchi, kupotea kwa mimea na viumbe hai pamoja na kusababisha
athari za kiafya kwa wananchi hasa wanawake wanaotumia nishati hiyo kupikia.
Makori ametumia fursa hiyo kuipongeza Halmashauri
ya Wilaya ya Mbinga kwa kuwa mfano mzuri wa kuhakikisha Mbinga inaandika historia ya kuanza safari ya kuachana na
matumizi ya kuni, mkaa na nishati nyingine isiyofaa katika shule.













No comments:
Post a Comment