Meneja wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa (katikati) akiwa na Afisa Huduma Mwandamizi kwa Wateja MSD Kanda ya Kati, Juliana Mbogo (kulia) pamoja na Msimamizi wa ujenzi wa ghara la kisasa la kuhifadhia dawa linalojengwa Dodoma, George Emmanuel (kushoto) wakati wa kwenda kuona ujenzi wa ghara hilo unavyoendelea.
----------------------------------
Na Dotto Mwaibale, Dodoma
BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza kukabidhi dawa kwa wateja wake kwa kutumia
mfumo wa kielekitroniki hatua ambayo imerahisisha namna ya kufanya makabidhiano
hayo.
Hayo yamebainishwa Julai 3, 2024 na Meneja wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Dodoma Mwanashehe Jumaa wakati
akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea MSD Kanda hiyo kwa ajili ya
kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo Kanda ya Dodoma.
“MSD tumeanza kukabidhi dawa katika Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati
kwa mfumo wa Kielekitroniki na mfumo huo unafanywa kupitia dereva ambaye
anakwenda kukabidhi mzigo huo kwa kutumia simu yake ya mkononi,” alisema Jumaa.
Jumaa alisema dawa hizo zinapokabidhiwa kwenye Hospitali au kituo cha afya inashirikishwa kamati ya
afya ya kijiji au kitongoji husika na kufuata taratibu zote zilizowekwa.
Aidha waandishi hao wakiwa kanda hiyo ya MSD waliweza kutembelea ghara
kubwa la kisasa la kuhifadhia dawa pamoja na kwenda kuona ujenzi wa maghara
mengine yanayojengwa karibu na eneo la
ofisi ya MSD Kanda ya Dodoma.
Kwa Upande wake Afisa
Huduma Mwandamizi kwa Wateja MSD Kanda ya Kati, Juliana Mbogo, alisema kanda
hiyo inahudumia Mikoa miwili ya Dodona na Singida ambapo kwa Singida inahudumia
halmashauri saba huku Dodoma ikiwa Halmashauri 8 na Wilaya ya Kiteto ambayo
ina halmashauri moja.
Mbogo
alisema mkoa huo wa Dodoma MSD imepewa jukumu la kuhifadhi dawa na kuzisambaza.
Safari ya kwenda kujionea ujenzi wa ghara hilo ukiendelea.













No comments:
Post a Comment