Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza na Waislamu wa Msikiti wa Munawara kuhusu mal za Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) zinavyo hujumiwa.
.................................
Na Dotto Mwaibale
AFISA Tarafa ya Mungumaji katika Manispaa ya Singida, Othman Mzee amepiga
marufuku shughuli zote za ujenzi zinazofanyika katika eneo la Msikiti wa Masjid
Munawara uliopo Kata ya Misuna zinazodaiwa kufanywa na watu wanaotajwa kuwa ni
wavamizi.
Mzee alitoa agizo hilo alipofika kuzungumza na waumini wa dini ya kiislamu
baaa ya swala ya Ijumaa iliyofanyika jana katika msikiti huo kufuatia mgogoro
wa ardhi uliopo baadhi ya watu wanaodai kuwa eneo hilo ni lao.
" Ninatoa maagizo ya kusimamisha shughuli zote za ujenzi kwenye eneo
hilo na mtu yeyote anayedai kuwa eneo hilo ni la kwake nawaomba kuanzia
jumatatu wafik ofisi kwangu wawe na nyaraka zinazoonesha kuwa eneo hilo ni
lake," alisema Mzee.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza wakati wa ibada ya swala
ya Ijumaa aisema kumekuwe na changamoto ya mali za kislamuzilizopo chini ya
Baraza Kla Kiislamu )BAKWAA) Mkoa wa Singida kuvamiwa na watu ambao hawana hofu
ya Mungu.
Alisema wnaovaovamia maeneo hayo ni
waislamu wenyewe ambapo alieleza kuwa mali zote za waislamu zipo chini ya
Baraza la Wadhamini na si vinginevyo
Sheikh wa Kata ya Misuna, Omari Is-Haka alisema kumekuwa na changamo kubwa
ya watu kuvamia maeneo ya msikiti iliyopo chini ya BAKWATA jambo ambalo
halikubaliki.
Alisema maeneo yote ambayo yanavamiwa ni mali halali ya BAKWATA na kuwa
yana nyaraka na hatimiliki.
Omari Lissu ambaye anadai kuwa maeneo hayo yanayodaiwa kuwa ni ya BAKWATA
ni ya kwao na yalikuwa yakimilikiwa na babu zake wanne ambao amewataja kwa jina
moja moja akianza na Digina, Mumwi, Mgiha na
Lissu ambaye i babu aliyemzaa baba yake.
Alisema kama familia eneo ulipojengwa msikiti na madrasa walilitoa kwa
waislamu kama walivyoomba na Sheikh wa Mkoa wa Singida wa wakati huo, Sheikh
Mahame lakini kuna eneo la Nasari bado ni la lao na ndilo wanalogombania
Lisu alisema anavielelezo vyote kuhusu eneo hilo mpaka ramani ambayo ipo
ofisi ya ardhi mkoa na kuwa atasimama kidete kuhakikisha haki yao inapatikana
kwani kuna baadhi ya watu wanania hofu ya kutaka kuwapoka eneo hilo
alililoachiwa mama yao mwenye miaka 87 na baba yao Mzee Issa Lissu ambaye kwa
sasa ni marehemu.
Aidha Lissu alikana familia hiyo kupewa viwanja 12 vilivyotolewa na ofisi ya ardhi kama mbadala wa eneo hilo ambalo lilipimwa kwa ajili ya taasis ya dini.








No comments:
Post a Comment