Diwani wa Kata ya Mkwese iliyopo Halmashauri ya Wilaya Manyoni Mkoa wa Singida Mhe. Ng'wigulu Shigella (katikati kushoto) akiwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza wa Shule ya Sekondari ya Mpambaa wakati wa hafla ya kuwakabidhi vifaa vya shule iliyofanyika Januari 14, 2026.
...........................
Na
Dotto Mwaibale
KUJITOA
kusaidia watu wengine ni jambo jema na pia ni kitendo cha baraka kutoka kwa
Mwenyezi Mungu.
Baadhi
ya watu wanafikiri kutoa msaada wowote ni lazima uwe mkubwa kumbe msaada hata
ukiwa mdogo kutokana na uwezo wa mtoaji kwa mpokeaji utakuwa mkubwa.
Kutoa
ni moyo wa mtu na siyo utajiri hivyo tupaswa kujenga tabia ya kutoa msaada kwa
wenzetu kama vitabu vitakatifu vya dini
zote vinavyotuelekeza.
Tabia ya kutoa inalinda na kuheshimu utu wa mtu kwa kumpatia chakula,
malazi, mavazi, huduma za afya, vifaa vya shule na mahitaji mengine ya
kibinadamu ambayo yanadumisha upendo, amani na mshikamano miongoni mwa
jamii.
Hapa
napenda nimzungumzie Diwani wa Kata ya Mkwese
iliyopo Halmashauri ya Wilaya Manyoni Mkoa wa Singida Mhe. Ng'wigulu Shigella.
Diwani huyu kupitia Chama
Cha Mapinduzi (CCM) ndiyo kwanza ameanza kazi rasmi ya kuwatumikia wananchi wa
kata hiyo kwa vitendo huku akishirikiana nao kwa kila jambo.
Kutokana na kuwiwa
kuwatumikia wananchi wake jicho la utumishi wake hasa katika majira haya ya msimu wa
watoto kwenda shule aliona aungane na baadhi ya wazazi na walezi ambao watoto
wao wanaenda kuanza kidato cha kwanza kwa kuwanunulia vifaa vya shule.
vifaa vilivyotolewa na kukabidhiwa kwa watoto hao 109 ni daftari
aina ya “Counter Book” sita kwa kila mwanafunzi,
Watoto walionufaika na
msaada huo ni ambao wameanza kidato cha kwanza Shule ya Sekondari ya Mpambaa iliyopo katika kata
hiyo.
Akizungumza wakati wa
kukabidhi msaada huo Shigella alisema ameona aungane na wazazi na walezi wa
watoto hao kwa ajili ya kusaidia vifaa hivyo vichache kwa kuwapa watoto hao ikiwa
kama motisha kwao ya kuanza kidato cha kwanza.
“Watoto wetu ndiyo mnaanza
masomo ya kidato cha kwanza wito wangu zingatieni masomo yenu hasa ya mchepuo
wa sayansi ambayo ndiyo msingi mzuri wa maendeleo yenu
na kufuata mnachoelekezwa na walimu wenu
msijiingize kwenye vitendo visivyofaa,” alisema Shigella.
Aidha, Shigella alisema msaada huo ulikuwa mahsusi
kwa ajili ya kuwaunga mkono wazazi na walezi
ambao wameonesha jitihada za kuwasimamia watoto wao vizuri hadi kufikia
hatua ya kuanza kidato cha kwanza.
Diwani
Shigella alisema pia amefanya hivyo ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anahimiza elimu
bure kwa watoto kuanzia shule ya awali hadi sekondari hivyo kuwapunguzia wazazi
mzigo wa kuwasomesha na kueleza kuwa utaratibu huo utakuwa endelevu kila mwaka.
m he. Shigella akikabidhi vifaa hivyo.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Shigella wakati wa kukabidhiwa vifaa hivyo.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990










No comments:
Post a Comment