Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga, akielekeza jambo wakati wa ukaguzi wa miradi ya elimu na afya katika katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi Januari 28, 2026.
.............................................
Na Mwandishi Wetu, Singida.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatma Mganga amefanya ziara ya
kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, kwa lengo la kukagua
utekelezaji wa miradi ya elimu na afya vilevile kuhakikisha matumizi
sahihi ya fedha za umma huku akiwataka wazazi na viongozi kuhakikisha
watoto wanapata haki yao ya Elimu na kushiriki kikamilifu katika
Mpangilio wa Lishe.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mganga akiiongoza timu ya ukaguzi amekagua
miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Zahanati ya Kitongoji cha Mlongoji,
unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na wananchi.
Serikali Kuu imetoa Tsh 50,000,000 kwa ajili ya umaliziaji wa
zahanati hiyo, huku wananchi wakichangia Tsh 2,614,000, wadau Tsh
2,750,000 na nguvu kazi yenye thamani ya Tsh 1,250,000. Aidha, Mfuko wa
Jimbo ulitoa Tsh 10,000,000 na hadi sasa, jumla ya Tsh 13,437,815.51
tayari imetumika.
Kwa upande wa miradi ya elimu miradi iliyokaguliwa, ni pamoja na
ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Kitaraka
unaofadhiliwa kupitia Programu ya BOOST kwa gharama ya Tsh 92,000,000.
Miradi ya elimu iliyokaguliwa, ni pamoja na ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Kitaraka.
Hadi sasa Tsh 69,055,299 tayari zimetumika. Mradi huo unatarajiwa
kunufaisha wanafunzi 667. Katika Shule ya Msingi Kazikazi, kamati
ilikagua ujenzi wa madarasa ya awali na msingi pamoja na matundu ya
vyoo, mradi unaogharimu Tsh 120,000,000 kupitia Programu ya BOOST.
Aidha katibu tawala huyo ameongoza timu yake hiyo ya ukaguzi
aliyoambatana nayo kukagua mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya
Kijobolo iliyopo Kitongoji cha Milumbi, unaotekelezwa kwa ushirikiano wa
Serikali na wananchi.
Mradi huo umefadhiliwa na michango ya wananchi, Mfuko wa Jimbo,
Halmashauri ya Wilaya ya Itigi na Programu ya BOOST kwa jumla ya zaidi
ya Tsh 300,000,000, ambapo hadi sasa zaidi ya Tsh 214,000,000 tayari
zimetumika.
Dkt. Fatma Mganga na timu yake wakiendelea na ukaguzi wa miradi.
Ni chombo cha habari kinachotoa habari na matukio mbalimbali nchini Tanzania na kokote duniani ,kwa kujali weledi na taaluma ya habari.
KWA MATANGAZO NA HUDUMA YA HABARI, WASILIANA NASI,
0754 362 990.
0688 914 344
Email: singidani77@gmail.com,
No comments:
Post a Comment