Naitwa Elias, mkazi wa jiji la Mwanza, maarufu kama mji wa
miamba. Kwa miaka saba, nilikuwa nikijishughulisha na biashara ya kuuza nguo za
mitumba na mpya katika soko kuu. Kila asubuhi nilikuwa nawahi kufungua duka
langu nikiwa na matumaini makubwa, lakini hali ilikuwa ya kusikitisha.
Nguo zangu zilikuwa ni nzuri na za kisasa, lakini cha ajabu
wateja walikuwa wakipita mbele ya duka langu na kuingia kwa jirani yangu ambaye
alikuwa na nguo za kawaida sana.
Nilikuwa nakata tamaa kila kukicha. Ilichukua muda mrefu sana hata kupata mteja mmoja wa kununua shati la shilingi elfu tano. Nilijaribu kila mbinu; nilipunguza bei, nilifanya matangazo madogo madogo, na hata kubadilisha mpangilio wa duka langu mara kwa mara, lakini hali ilibaki kuwa ileile.








No comments:
Post a Comment