Naitwa Sylvester, mkazi wa zamani wa wilaya ya Ubungo, jijini
Dar es Salaam. Kwa miaka mitano nilikuwa nimefungua ofisi ya stationary (huduma
za kompyuta na kupiga picha). Licha ya kuwa katikati ya vyuo na ofisi nyingi,
duka langu lilikuwa kama limepakwa pilipili; wateja walikuwa wakichungulia na
kupita zao.
Nilikuwa naishi maisha ya ajabu, nakula mlo mmoja kwa siku –
tena usiku kama daku – ili tu nisife na njaa. Nilianza kuonekana mzee kabla ya
umri wangu kwa sababu ya mawazo ya kodi na mikopo.
Kila nikijaribu kuleta mashine mpya ili kuvuta wateja, mashine hiyo ilikuwa inaharibika ndani ya wiki moja. Nilihisi nina nuksi ambayo siyo ya kawaida. Nilianza kuwaogopa hata ndugu zangu nikihisi ndio wamenizibia milango ya riziki. Nilikaribia kufunga ofisi na kwenda kuwa bawaba (mlinzi) wa usiku ili tu nipate pesa ya pango la chumba.








No comments:
Post a Comment