Naitwa Shadrack, mkazi wa zamani wa jiji la Mwanza. Kwa
zaidi ya miaka sita, nilikuwa nimefungua duka la nguo za kisasa (boutique)
maeneo ya mtaa wa Liberty. Licha ya kupata mzigo mpya kila mwezi kutoka
Nairobi, duka langu lilikuwa kama limepakwa dawa ya kufukuza watu.
Nilikuwa nafika asubuhi, napangusa vioo, kisha nashinda
nimekaa mlangoni nikifukuza nzi na kutazama watu wakipita bila kuingia ndani.
Nilianza kuonekana kituko, huku mke wangu akianza kunidharau kwa kushindwa
kutoa hata hela ya mboga.
Hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba nilianza kukopa hadi kwa jirani anayeuza genge ili nipate nauli ya kurudi nyumbani. Nilihisi nina nuksi iliyogandishwa na mtu mwenye kijicho. Nilijaribu kufanya ofa za ‘buy one get one free’, lakini bado watu walikuwa hawaji. Nilikonda kwa mawazo na kila usiku nilikuwa naliota duka langu likiungua moto – ishara tosha kuwa mambo yalikuwa yamefika ukingoni.








No comments:
Post a Comment