Kulikuwa na tukio la kushangaza sana katika eneo la Temeke jijini Dar es Salaam baada ya kijana mmoja kudaiwa kuiba pikipiki na ghafla kuanza kuimba nyimbo za kanisani katikati ya barabara bila kukoma. Tukio hilo lilivuta umati mkubwa wa watu waliokuwa wakishuhudia hali hiyo isiyo ya kawaida.
Kwa mujibu wa mashuhuda, kijana huyo aliiba pikipiki iliyokuwa imeegeshwa nje ya duka na kuondoka kwa kasi. Hata hivyo, baada ya kufika umbali mfupi, ghafla alipunguza mwendo, akasimama, na kuanza kuimba nyimbo za kanisani kwa sauti kubwa bila kujali watu waliokuwa wakimwangalia.








No comments:
Post a Comment